Sunday, November 20, 2016

MEYA ARUSHA: PAZENI SAUTI WABUNGE WAWE NA "DEGREE''

Mea wa jiji la Arusha Calist Lazarro
Ameyasema hayo mapema jana alipokuwa akiwatunuku wahiti wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha[AJTC[ ngazi ya stashahada mahafali yaliofanyika katika ukumbi wa PPS jijini Arusha nakuwataka waandishi wa habari kupaza sauti ili wabunge wawe na elimmu ya ngazi ya  Shahada.

Amesema kuwa  sheria ya mwaka 2016 iliyowekwa na wabunge hivi karibuni imemkandamiza Mwandishi wa Habari kwani inamtaka awe na kiwango cha elimu ya Shahada ndipo atambulike kama mwanahabari, ivyo wanaotunga sheria hizo ni wabunge ivyo nao wawe na Elimu yakutosha wawapo Bungeni.


Aidha Lazarro alitoa  rai kwa waandishi wa habari waliohitimu pamoja na walioko katika vyombo vya habari kuwa wazitumie kalamu zao kuwatetea wanyonge pamoja na kufanya kazi katika maadili ili kuepukana na kesi za kuvunja sheria mpya zilizowekwa na wabunge  hivi karibuni
Wahiti wa Arusha journalism Training College


Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi waliohitimu hapo jana Bwana Underson Bugoma amesema anamshukuru mungu kwa kumjalia kuhitimu masomo yake salama na kuhaidi atakuwa mwandishi makini na kusimamia ukweli na si kinyume na hapo...

Aidha mmoja wa wanafunzi anayesalia chuoni hapo Bi Asha Kabuga ameeleza kusikitishwa na kuhitimu kwa wanafunzi hao lakini ameeleza kuwa pamoja na kuwapenda na kuwazoea wao bado watawahitaji ili kufika mbali zaidi katika tasnia.


Chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha ni miongoni wa vyuo ambavyo vinatoa mafunzo bora ya uandishi wa habari na utangazaji nchini  na kinashika nafasi ya pili Tanzania kwa mujibu wa NACTE.

NEC yatoaelimu ya mpiga kura Songea Girls





Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mstaafu Mary Longway (kushoto) akisaini kitabu cha wageni cha Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea baada ya kufika Ofisi ya Mkuu wa Shule hiyo Tupoke Ngwala (katikati).Kulia ni Mratibu wa Uchaguzi mkoa wa Ruvuma, Joel Mnemba.



Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea, Tupoke Ngwala (aliyevaa nguo ya kitenge) akitambulisha wageni kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa wanafunzi wa shule hiyo.Kulia ni Kamishna wa Tume hiyo Mhe. Jaji Mst. Mary Longway.



Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mst. Mary Longway akiwasalimia wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea baada ya kuwasili shuleni hapo kwa ajili ya kutoa elimu ya mpiga kura.



Ugeni kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi na meza kuu, ikiongoza wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea kuimba wimbo wa Taifa baada ya kufika ukumbi wa mikutano wa shuel hiyo kwa ajili ya kutoa elimu ya mpiga kura.



Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea wakiimba wimbo wa shule hiyo.



Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mst. Mary Longway akitoa utangulizi wa elimu ya mpiga kura.Kushoto ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea, Tupoke Ngwala na kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria Bw. Emmanuel Kawishe.



Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria Bw. Emmanuel Kawishe akiwasilisha mada ya Elimu ya Mpiga Kura kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea. Kulia kwake ni Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mst. Mary Longway na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea, Tupoke Ngwala.



Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea wakifuatilia elimu ya mpiga kura.





Baadhi ya walimu wa wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea wakifuatilia elimu ya mpiga kura.



Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea wakiuliza maswali baada ya kupata elimu ya mpiga kura.



Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji Mst. Mary Longway akimkabidhi Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea Tupoke Ngwala, Taarifa ya Tathmini Baada ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani wa mwaka 2015, baada ya kuhitimisha elimu ya mpiga kura.



Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea Tupoke Ngwala akitoa neno la shukrani.

Picha na Hussein Makame, NEC

………………………………………………………………………

Hussein Makame, NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa Elimu ya mpiga Kura katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Songea mkoani Ruvuma na kueleza umuhimu wa elimu hiyo katika kuwawezesha wananchi na wadau wa uchaguzi kufahamu taratibu na hatua zote za uchaguzi hadi kutangazwa kwa matokeo.

Akitoa utangulizi wa elimu hiyo, Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mst. Mary Longway aliwataka walimu, wanafunzi na watumishi wa shule hiyo waliopata elimu hiyo wakawe mabalozi wa kuifikisha elimu ya mpiga kura kwa jamii inayowazunguka.

“Binafsi nategemea kila mmoja wenu ataweza kumuelimisha mwenzake ambaye hakupata nafasi kama hii ya kujua ni nini elimu ya mpiga kura” alisema Mhe. Jaji Mst. Longway.

Alisema Elimu ya mpiga kura ikitolewa humuwezesha mwanafunzi ambaye ni mpiga kura na mgombea mtarajiwa kufahamu sifa za kuandikishwa kuwa mpiga kura au mgombea.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Tume hiyo Bw. Emmanuel Kawishe alifafanua baadhi ya vipengele mbalimbali kuhusu uchaguzi ikiwemo kuweka utaratibu wa mtu kupiga kura kwenye kituo au eneo alilojiandikishia.

Alisema Kifungu cha 61 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinamruhusu mtu kupiga kura kwenye kituo alichojiandikisha na kwamba utaratibu huo huepuka baadhi ya sehemu kuwa na wapiga kura wengi kuzidi uwezo wakati vituo vingine vikikosa kabisa wapiga kura.

Akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo, Bw. Kawishe alizungumzia elimu ya mpiga kura kwa baadhi ya jamii zinazoishi maisha ya kuhamahama sehemu tofauti.

Alisema Tume inawajali wananchi wanaoishi kwa kuhamahama na inawafikia wananchi hao kupitia ushirikishwaji wa asasi za kiraia zinazokwenda kutoa elimu katika maeneo ya jamii hizo ili kuwafikia wananchi ambao ni ngumu kuwafikia.

“Wakati mwingine ili kuyafikia makundi hayo ya wananchi Tume inatumia ngoma na vikundi vya kiutamaduni kwenye maeneo husika, tunatumia redio za jamii za maeneo yale, kwa hiyo asipopata elimu kwa njia hii ataipata kupitia redio na njia za kitamaduni” alisema Bw. Kawishe.

Baadhi ya wanafunzi walizungumzia Elimu hiyo walisema wameridhishwa na Elimu waliyoipata na imewasaidia kufahamu mambo mengi yanayohusu Uchaguzi.

“Kwa kweli sisi wanafunzi wa Songea Girls tumefurahishwa sana kwa kupata elimu ya mpiga kura kwa kuwa imetusaiodia kujua haki zetu kama Watanzania hasa katika masuala ya uchaguzi” alisema mwanafunzi Faraja Samwel Sanga.

Kwa upande wake Husna Banda alisema amefurahi kupata elimu kuhusu kupiga kura na pia amejua umuhimu wa kupiga kura kumchagua kiongozi ambaye anampenda kwa ajili ya maedeleo ya taifa lake.

Akitoa neno la shukrani, Mkuu wa Shule hiyo Tupoke Ngwala alisema wanashukuru kwa nafasi ambayo wameipata ya kupata elimu ya mpiga kura na kwamba anaamini itakuwa msaada mkubwa kwa maendeleo ya nchi na kuahidi kuifanyia kazi kwa kadri ya uwezo wao ili kufikia lengo lililokusudiwa.

WAZIRI WA UTAMADUNI NA SANAA WA AFRIKA YA KUSINI ATEMBELEA KITUO CHA MAENDELEO DAKAWA NA MAKABURI YA WAPIGANIA UHURU WA CHAMA CHA ANC MKOANI MOROGORO.





Kaimu Mkurugenzi kituo cha Maendeleo Dakawa Bw. Elasto Nywage(kulia) akitoa maelezo ya kituo hicho kwa Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa wakati Waziri huyo na ujumbe wako walipotembelea kituo hicho na kujionea makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC.



Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akizungumza na viongozi wa Kituo cha Maendelo Dakawa (hawapo pichani) wakati Waziri huyo na ujumbe wake walipotembelea kituo hicho na kujionea makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC.



Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa(katikati) akiangalia makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC yaliyopo Dakawa wilayani Kilosa mkoani Morogoro.



Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa(katikati) akiangalia makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC yaliyopo Dakawa wilayani Kilosa mkoani Morogoro.



Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa akiweka shada la maua katika eneo maalum katika makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC yaliyopo Dakawa wilayani Kilosa mkoani Morogoro.



Eneo la makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC yaliyopo Dakawa wilayani Kilosa mkoani Morogoro.



Kaimu Mkurugenzi kituo cha Maendeleo Dakawa Bw. Elasto Nywage(kulia) akimuonesha Waziri wa Utamaduni na Sanaa wa Afrika ya Kusini Mhe. Nathi Mthethwa(katikati) bango linaloelezea kuwa eneo hilo ndipo yalipo makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC katika wilayani Kilosa mkoani Morogoro.



Bango linaloelezea kuwa eneo hilo ndipo yalipo makaburi ya wapigania Uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka Chama cha ANC wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

TIMU YA GOLF YA JWTZ YA LUGALO YAWEKA HESHIMA KATIKA GOLF YANYAKUA KOMBE LA WAITARA





Mshindi wa Jumla wa kombe la Mkuu wa Majeshi Mstaafu George Waitara, kutoka klabu ya Lugalo Juma likuli akiwa amenyenyua vikombe alivyokabidhiwa na Jaji Mkuu Mh Othman Chande aliyekuwa mgeni rasmi katika mashindano hayo yaliyofanyika Jumamosi Novemba 19 jijini Dar es salaam.(Picha na Luteni Selemani Semunyu).



Mshindi wa Kundi la Wanawake wa kombe la Mkuu wa Majeshi Mstaafu George Waitara, kutoka klabu ya Lugalo Sophia Mathias akipokea zawadi ya Meza aliyekabidhiwa na Mke wa Jenerali Mstaafu Waitara katika mashindano hayo yaliyofanyika Jumamosi Novemba 19 jijini Dar es salaam.(Picha na Luteni Selemani Semunyu).



Mkuu wa Majeshi Mstaafu George Waitara,kulia akibadilishana Mawazo na wachezaji mwenzi ambaye ni katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana (katikati) katika mashindano yaliyofanyika Jumamosi Novemba 19 jijini Dar es salaam kushoto ni katibu mkuu Wizara ya ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima.(Picha na Luteni Selemani Semunyu).



Mwenyekiti wa Klabu ya Lugalo brigedia Jenerali Michael Luwongo akiwa ameshika zawadi ya kikombe alichokabidhiwa na Chama cha Golf Tanzania TGU ikiwa ni ishara ya Kutambua Mchango wa Klabu hiyo katika kukuza mchezo wa Golf Nchini kulia ni mweka hazina wa TGU Akhil Yusuphali mara baada ya mashindano ya Waitara yaliyofanyika Jumamosi Novemba 19 jijini Dar es salaam.(Picha na Luteni Selemani Semunyu).akhil yusuphali



Mkuu wa Majeshi Mstaafu George Waitara,kulia akibadilishana Matokeo na wachezaji wenzie,katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana (kushoto) na katibu mkuu wizara ya ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh Job Masima katikati katika mashindano ya Waitara Trophy Jumamosi Novemba 19 jijini Dar es salaam.(Picha na Luteni Selemani Semunyu).

……………………………………………………………………..
Na Luteni Selemani Semunyu
Timu ya Golf ya Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania ya Lugalo imeweka heshima katika mchezo huo baada ya kunyakua Ubingwa wa kombe la mkuu wa majeshi Mstaafu George Waitara kwa mara ya tatu katika mashindano yaliyochezwa Jumamosi Novemba 19 Jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya Mchezaji wake Juma Likuli kuibuka mshindi wa Jumla baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 66 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni Tano na kuwashinda Wachezaji zaidi ya 100 kutoka vilabu mbali mbali nchini waliojitokeza kushiriki mashindano hayo.

Katika Divisheni A Cloud Mtavangu wa Lugalo aliibuka na ushindi kwa Mikwaju ya Jumla 67 baada ya kupiga mikwaju 74 na kiwango chake cha Uchezaji Kikiwa ni saba na kufuatiwa na Hendrick Nyenza wa Lugalo kwa CountBack baada ya kupiga mikwaju ya Jumla 68 huku kiwango chake cha Uchezaji Kikiwa ni Tatu.

Katika Divisheni B Iddi Ramadhani wa Lugalo aliibuka na Ushindi Baada ya Kupiga Mikwaju ya Jumla 67 huku kiwango chake cha Uchezaji Kikiwa ni 18 akifuataiwa na Noel Mheni wa Lugalo baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 69 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 15.

Katika Divisheni C mpiga golf A, Ngamilo wa klabu ya Gymkhana ya Dar es Salaam aliibuka na Ushindi baada ya Kupiga Mikwaju ya Jumla 74 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 24 akifuatiwa na Alfred Kinswaga wa Lugalo baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 75 huku kiwango chake cha Uchezaji Kikiwa ni 20.
Kwa upande wa Senior Mpiga Golf Saidi Nkya wa Lugalo aliibuka na Ushindi baada ya kupiga Mikwaju ya Jumla 73 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 15 akifuatiwa na Boniface Nyiti wa Lugalo aliyepiga mikwaju ya Jumla 74 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni Nane .

Kwa upande wa kundi la Wanawake Sophia Mathias wa Lugalo aliibuka Na ushindi baada ya Kupiga Mikwaju ya Jumla 74 huku kiwango chake cha Uchezaji kikiwa ni 13 akifuatiwa na Vicky Elias aliyepiga Mikwaju ya Jumla 76 huku kiwango cha Uchezaji Kikiwa ni Tisa.

Kwa Upande wa Wachezaji wa kulipwa Nuru Mollel wa Klabu ya Gymkhana ya Arusha aliibuka na ushindi na katika kundi la Wachezaji wasaidizi Robert Jamson aliibuna na Ushindi kwa Mikwaju ya Jumla 65 akifuatiwa na Gerad Gadiel.

Hili linakuwa kombe la pili kuchukuliwa moja kwa moja na klabu ya Lugalo baada ya kutimiza vigezo vya kulinyakua mara tatu mfululizo baada ya pia Kombe la mkuu wa majeshi CDF TROPHY ambalo nalo sasa limeenda moja kwa moja kwa Lugalo na mwakani inapaswa kutafutwa makombe mapya.